Kupitisha (Adoption) katika Hizb ut-Tahrir

Baada ya utafiti, fikra na uchunguzi kuhusu hali ya sasa ya Ummah na kuhusu hali iliyokuwa imefikia, na hali wakati wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw), na wakati wa Makhalifa wanne Waongofu na wakati wa wale waliowafuata, na kurejelea seerah na njia ambayo yeye (saw) alibeba da’wah tangu wakati alipoanza hadi alipoanzisha Dola huko Madinah; na baada ya kusoma njia ambayo yeye (saw) alifanya kazi huko Madinah na kwa kurejelea Kitabu cha Mwenyezi Mungu (swt), na Sunnah ya Mtume Wake (saw) na kwa yale waliyoyaashiria ya Ijma’ ya Masahaba na Qiyas, na maoni yaliyoelimika ya Masahaba na wafuasi wao, na maoni ya mujtahidiina, baada ya yote haya Hizb ut-Tahrir basi ilipitisha mawazo, maoni na sheria zinazohusiana na wazo na njia. Hayo si chochote ila ni mawazo, maoni na sheria za Kiislamu, hakuna chochote ambacho si cha Kiislamu, wala hayaathiriwi na chochote kisicho cha Kiislamu; badala yake si chochote ila ni ya Kiislamu na hayategemei chochote isipokuwa vyanzo vya Uislamu. Chama kinakimbilia kwenye fikra katika kuhitimisha mawazo, maoni na sheria hizi.

Hizb ilipitisha mawazo, sheria na maoni ambayo ni muhimu kwake ili kuendelea katika kazi ya kurejesha njia ya maisha ya Kiislamu na kubeba da’wah ya Kiislamu kwa ulimwengu kupitia uanzishwaji wa Dola ya Khilafah na kumteua Khalifah.

Chama kiliambatanisha yote kiliyoyapitisha na yaliyotolewa nacho ya mawazo, sheria na maoni katika vitabu vyake na katika vipeperushi vyake vingi ambavyo kilichapisha na kutoa kwa watu.

Vitabu Vilivyochapishwa na Chama

  1. Mfumo wa Uislamu
  2. Mfumo wa Utawala wa Uislamu
  3. Mfumo wa Uchumi wa Uislamu
  4. Mfumo wa Kijamii wa Uislamu
  5. Muundo wa Chama
  6. Dhana za Hizb ut-Tahrir
  7. Dola ya Kiislamu
  8. Haiba ya Kiislamu (katika juzuu tatu)
  9. Dhana za Kisiasa za Hizb ut-Tahrir
  10. Maoni ya Kisiasa ya Hizb ut-Tahrir
  11. Utangulizi wa Katiba
  12. Khilafah
  13. Jinsi Khilafah Ilivyovunjwa
  14. Kanuni ya Adhabu
  15. Sheria za Ushahidi
  16. Ukanushaji wa Ukomunisti wa Kimarx
  17. Fikra
  18. Uwepo wa Akili
  19. Fikra ya Kiislamu
  20. Ukanushaji wa Nadharia ya Dhima katika Sheria ya Magharibi
  21. Wito wa Joto
  22. Sera Bora ya Uchumi
  23. Hazina katika Dola ya Khilafah

Chama pia kimetoa maelfu ya vipeperushi, vikumbusho na vijitabu vya kifikra na kisiasa.

Mkabala wa Kisiasa

Wakati Chama kinapobeba dhana na sheria hizi kwa watu, kinazibeba kisiasa, yaani kinabeba dhana hizi kwao ili watu wazipitishe, wazifanyie kazi na kuzibeba ili kuziweka katika serikali na katika mambo ya maisha. Hii ni kwa sababu ni wajibu juu yao kama Waislamu, kama ilivyo wajibu kwa Chama kama chama cha Kiislamu, na wanachama wake kama Waislamu.

Vyanzo vya Kupitisha

Chama kinategemea katika kupitisha kwake mawazo na sheria za Kiislamu pekee juu ya ufunuo wa Qur’an, Sunnah, Ijma’ ya Masahaba na Qiyas, kwa sababu vyanzo hivi vinne ndivyo vyanzo pekee ambavyo uthibitisho wake umethibitishwa na ushahidi wa yakini.